
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.

Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Mhe. Freeman Mbowe.
--- 
 KIKAO cha
 Bunge leo kimeanza kwa maswali kwa Waziri Mkuu ambapo aliyekuwa wa 
kwanza kuuliza alikuwa ni Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, 
Mhe. Freeman Mbowe
“…Chini
 ya uongozi wako kama Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na 
ukiwa kiongozi wa shughuli za Kiserikali Bungeni, tumeiona Serikali 
ikikumbana na matatizo na vikwazo vingi ikiwemo ‘Operesheni Tokomeza’ 
ambayo ilipelekea wananchi wengi kupoteza maisha na wengine kupata 
vilema…“
Tumeona
 mauaji ya raia yakiendelea Kiteto, kashfa kubwa ambayo iko current sasa
 hivi ikiwa ni pamoja na kauli zako ulizowahi kuzisema kwamba fedha 
zilizopotea za akaunti ya Escrow hazikuwa fedha za umma bali zilikuwa 
fedha za watu binafsi…“– Mbowe.
Baada 
ya Ripoti ya CAG kutolewa hadharani kuhusiana na fedha za Akaunti ya 
Escrow na baada ya Ripoti ya PCCB kutolewa na hatimaye jana hapa Bungeni
 kusomwa taarifa ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), nini 
msimamo wako kuhusu kauli yako ya awali kwamba fedha zile zilikuwa ni za
 watu binafsi na sio fedha za umma?“– Mbowe.
Kwa 
uzito huo ukichanganya na matukio mengine mbalimbali ambayo yamepelekea 
fedheha kubwa kwa taifa letu, huoni kama ingekuwa muafaka kwako binafsi 
na taifa kupumzika kidogo ili kupisha nafasi kwa watu wengine kuweza 
kumalizia ngwe hii ya utawala wenu?”– Mbowe.
Akijibu
 maswali hayo, Waziri Mkuu Mizengo Pinda amesema; “…Inawezekana 
Mheshimiwa Mbowe una shauku ya kutaka litokee hilo lakini mambo haya 
yanategemea kama ndivyo Mungu kapanga au hapana…“
Ningeweza
 nikajaribu kukujibu lakini sina sababu ya kufanya hivyo, sina sababu ya
 kufanya hivyo kwa sababu suala lenyewe ndiyo subject ya mjadala hapa 
Bungeni ambao unaanza leo.. Tusubiri mjadala utakavyokwenda naamini na 
mimi nitapata nafasi ya kusema mawili matatu, kwa hiyo nadhani mwisho wa
 yote Bunge litakuwa limefikia mahali ambapo tunaweza tukasema kwa 
uhakika ni hatua stahiki namna gani inaweza kuchukuliwa…” Waziri Mkuu 
Mizengo Pinda.
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment