Home » » DODOMA YATINGA FAINALI KWA KISHINDO

DODOMA YATINGA FAINALI KWA KISHINDO

Dodoma imeiduwaza Kigoma baada ya kuichapa mabao 2-1 na kufanikiwa kutinga fainali ya mashindano ya Copa-Coca-Cola jana kwenye Uwanja wa Karuma, Dar es Salaam.
Hii ni mara ya kwanza kwa timu ya Dodoma kufuzu hatua hatua ya fainali tangu kuanzishwa kwa mashindano hayo 2007.
Mshujaa wa Dodoma katika mchezo huo  Juma Magid na Pius Raphael walifunga mabao mawili wakati Nashri Adam akifunga bao la kutokana na machozi kwa Kigoma.
Kocha wa Dodoma, Mussa Fiurutuni alisema  nimefurahi sana timu yangu kuingia hatua ya fainali kwa mara ya kwanza.
“Wachezaji wangu walicheza kwa ari kubwa na kujituma jambo lililochangia kupata ushindi huu, nimefurahi sana kwa kweli,” alisema kocha huyo.
Kigoma walipewa nafasi kubwa ya kuibuka bingwa wa mashindano haya ya mwaka huu walikuwa wa kwanza kupata bao dakika pili lililofungwa na Nashri Adam aliyeunganisha kwa umakini mpira uliopigwa na Shaban Maneno na kumwacha kipa wa Dodoma asijue la kufanya.
Baada ya bao hilo Dodoma iliamka na kusawazisha dakika ya 19 kupitia kwa Juma Magid kwa kichwa baada ya kuunganisha mpira wa adhabu ndogo na kufanya timu hizo kwenda mapumziko zikiwa sare 1-1.
Dodoma ilianza kipindi cha pili kwa kasi na kufanikiwa kupata bao la pili dakika 49 kupitia kwa Pius Raphael aliyepiga shuti lililomshinda kipa Kigoma, Bashiri Twalib.
Kocha wa Kigoma, Hamis Mabo alisema makosa machache yaliyofanywa na safu yake ulinzi yameigharimu timu yake.
“Kusema ukweli wa kujilaumu ni sisi wenyewe kutokana na makosa tuliyofanya, ila kikubwa ndiyo matokeo yalivyo na ni lazima tukubaliane nayo,” alisema Mabo.
Dodoma ilifanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali baada ya kuifunga Morogoro kwa mabao  2-1, mchezo uliochezwa kwenye Uwanja wa Tanganyika Packers, Kawe huku Kigoma ikiifungasha virago Mwanza kwa bao 1-0 kwenye Uwanja wa Karume.
Mashindano haya ya vijana yanayofanyika kila mwaka nchini yana lengo la kuibvua vipaji vipya katika mwendelezo wa ukuzaji wa soka la Tanzania.
Kampuni wadhamini wa mashindano haya, Coca cola huleta wakufunzi kila mwaka nchini kwa ajili ya vijana wanaounda timu ya kombaini na kuangaliwa kabla ya kwenda kuendelezwa katika vituo vya nje.
Chanzo:Mwananchi
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa