Home » » SERIKALI YAFAFANUA SUALA LA TAASISI ZA SERIKALI KUFUNGUA AKAUNTI BOT

SERIKALI YAFAFANUA SUALA LA TAASISI ZA SERIKALI KUFUNGUA AKAUNTI BOT

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema.
Serikali  imesema uamuzi wa kuyataka mashirika ya umma pamoja na taasisi za serikali kufungua akaunti Benki Kuu (BoT) itasaidia kupunguza riba kwenye benki.
 
Akizungumza bungeni jana wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema, Waziri wa Fedha, Dk. Philip Mpango, alisema serikali kupitia Benki Kuu itaendelea kusimamia sekta ya fedha ili kuhakikisha riba zinapungua kwenye mabenki.
 
Alisema katika mapendekezo ya mpango waliouwasilisha, moja ya hatua ambazo serikali inachukua ni kuhakikisha taasisi za umma zinafungua akaunti katika Benki Kuu.
 
Alisema lengo la kufanya hivyo ni  kuhakikisha fedha nyingi zilizokuwa zinatumiwa na mabenki kwa ajili ya kufanya biashara bila serikali kupata faida sasa zinatumika ili mabenki hayo yaende vijijini kupeka huduma kwa wananchi.
 
“Hii ni hatua moja wapo ya kusaidia kupunguza riba ili wananchi wetu waweze kunufaika zaidi,” alisema.
CHANZO: NIPASHE

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa