Home » » Wahudumu wa afya wanaotoa lugha chafu kwa wagonjwa kwenda jela

Wahudumu wa afya wanaotoa lugha chafu kwa wagonjwa kwenda jela

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Serikali imesema wahudumu wa afya ambao bado wanatoa lugha chafu kwa wagonjwa watafikishwa katika mabaraza ya wauuguzi na phamasia ambapo ili kutoa maamuzi ikiwemo kuwafikisha mahakamani pale itakapobainika makosa ni makubwa kwa wahudumu hao.

Hayo yamesemwa Bungeni Dodoma katika kikao cha Bunge ambapo Naibu waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Khamis Kigwangalla alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti maalum CCM Faida Mohamed Bakari.


Mbunge Farida ametaka kujua namna serikali ilivyojipanga kutokomeza tabia mbaya ya wahudumu wa afya hasa kutoa lugha chafu kwa wagonjwa hususani kwa kinamama wajawazito.

''Ni marufuku kwa wauguzi kutoa lugha chafu kwa wagonjwa na wana bodi zao za taaluma zao hivyo kila mgonjwa anaehudumiwa aangalie anahudumiwa na nani na atoe maoni yake katika eneo husika ili sheria ichukue mtandao wake''Amesisitiza Dkt.Kigwangalla.

Dkt.Kigwangalla amesema wizara yake pia imeandaa utaratibu maalumu wa kutoa semina kwa wakunga wa jadi ili waweze kutoa huduma vijijini kwa utaratibu utakao leta tija zaidi.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa