Home » » Madiwani wapigiwa chapuo taarifa za mchakato wa manunuzi

Madiwani wapigiwa chapuo taarifa za mchakato wa manunuzi

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, Hawa Ghasia

KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti imeishauri serikali kuweka utaratibu maalumu kwenye kanuni za sheria ya manunuzi kuruhusu baraza jipya la madiwani kupewa taarifa ya mchakato wa manunuzi kwa kipindi chote wakati baraza halikuwepo.
Ushauri huo unatokana na kamati hiyo kubaini kwamba kuna mapungufu makubwa katika manunuzi ya umma hasa katika kipindi cha uchaguzi wakati Kamati ya Fedha pamoja na Baraza la Madiwani huwa limevunjwa.
Akitoa taarifa kuhusu Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Ununuzi wa Umma wa Mwaka 2016 uliowasilishwa juzi, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Hawa Ghasia alisema kwa sasa kanuni za uendeshaji wa halmashauri haziruhusu Baraza la Madiwani kujadili taarifa ya manunuzi na taarifa nyingine pindi baraza jipya la madiwani linapoingia.
Ghasia alisema kwa hali ilivyo inafaa kuwepo kwa kanuni inayotoa ruksa kwa baraza jipya ili kuziba mianya ya manunuzi holela kipindi cha Uchaguzi Mkuu.
Aidha, kamati hiyo imeitaka serikali wakati wa kuandaa kanuni kuzingatia mazingira wezeshi yatakayosaidia wahisani wanaochangia miradi ya maendeleo pale wanapohitaji serikali iwasaidie kugharamia baadhi ya michango au huduma za haraka ambazo zitasaidia utekelezaji wa mradi husika.
“Mfano wahisani wanaweza kutoa msaada wa vifaa vya hospitali kwa masharti kwamba serikali itahitaji kuchangia bima na usafirishaji. Fursa hizi zionenshwe kwenye kanuni hasa kwa upande wa miradi ya ubia (PPP) itakayohusu ujenzi wa madarasa, barabara na miundombinu mingine katika halmashauri na Serikali Kuu,” alifafanua Ghasia.
Pia kamati ilishauri serikali kuhakikisha kuwa taasisi za serikali zinatoza bei ya soko ili zishindane katika soko na kupata wateja zaidi kuliko sasa.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa