ULEDI MUSSA: KUNA
UHURU MKUBWA SANA NDANI YA BUNGE
Na Daudi
Manongi,MAELEZO
Katibu
Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Bunge Bw.Uledi Mussa
amesema kuwa wabunge wana uhuru mkubwa
sana wa kuzungumza ndani ya Bunge.
Katibu
Mkuu uyo ameyasema hayo katika kipindi cha TUNATEKELEZA leo jioni
kinachoandaliwa na Idara ya Habari MAELEZO na kurushwa na TBC1.
“Bunge
letu liko huru sana,liko huru kwa maana wabunge wana uhuru wa kuzungumza na
kikatiba yale wanayozungumza ndani ya bunge hawawezi kushitakiwa nje,kwa maana
hiyo kuna uhuru mkubwa sana,lakini sasa bunge lenyewe lina Kanuni zake ambapo
wewe uliye ndani ya Bunge usimseme mtu ambaye hana fursa ya kuzungumza ndani ya
Bunge hivyo bungeni msingi wake mkubwa
ni kuzungumza hoja pamoja na kuikosoa,kuishauri serikali na tunafatilia ushauri
huu kisekta ili ufanyiwe kazi”Alisema Bw.Uledi
Akizungumzia
suala la utoro Bungeni amesema kuwa kwa sasa mahudhurio yanaratibiwa
kielektronikali na wabunge watapaswa
kuweka dole gumba kwenye mshine
ili ajulikane kaingia na kutoka na baadae mahudhurio hayo uchambuliwa na
kutumwa katika vyama vyao na hivyo ili litaongeza uwajibikaji binafsi kwa
wabunge.
Akizungumzia
upande wa hali ya vyama vya siasa nchini katibu mkuu uyo amesema kuwa vyama vingi vya
siasa bado ni vichanga na msingi wa vyama vingi hauna muda mrefu hivyo bado vina kazi kubwa ya kujijenga
vyenyewe kama taasisi kwenye kuchagua viongozi na Katiba zao.
Aidha
katibu Mkuu uyo amevitaka vyama vya siasa kujenga misingi ya kukubali matokeo
ya chaguzi zinapofanyika na pia vijenge umoja unaozingatia katiba za vyama
vyao.
Bw,Uledi
pia amesisitiza kuwa matatizo yanayotokea ndani ya vyama vya siasa yanapaswa kutatuliwa na vyama na wanachama wao wenyewe
na kuongeza kuwa migogoro mingi ndani ya vyama ni ya kikatiba na hivyo wasitegemee mtu kutoka nje aje
kuwatatulia matatizo yao ingawa ofisi ya waziri mkuu itaendelea kushirikiana na
msajili wa vyama vya siasa katika kuwa mlezi wa vyama hivi.
0 comments:
Post a Comment