Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Timu
ya utambulisho wa Mradi wa kuchora Ramani za kijiografia kutoka Korea
na baadhi ya watendaji wa Idara ya Upimaji wa Ramanni (Wizara ya Ardhi)
katika Mkutano wa utambulisho wa Mradi.
Ugeni
kutoka Taasisi ya Taifa ya Kijiografia- Korea, waliofika kutambulisha
Mradi wa kuchora Ramani za kijiografia utakaoanza 2018, katika picha ya
pamoja na baadhi ya watenfaji wa Wizara ya Ardhi.
Ugeni wa Wakorea, kutoka Taasisi ya
Taifa ya masuala ya kijiografia umetambulisha rasmi mradi wa kuchora ramani za
kijiografia kwa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.
Ugeni huo uliopokelewa na Idara ya
Upimaji na Ramani katika Wizara ya Ardhi, umehusisha timu ya Maafisa kumi
kutoka nchini Korea. Akizungumza na wawakilishi wa Idara ya Upimaji na Ramani; Naibu
Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango wa Taasisi hiyo; Bwn. Hynu-Hee Joo
amesema mradi huo unaojumuisha nchi tatu, yaani Tanzania, Zambia na Msumbiji
unategemewa kuanza rasmi 2018.
Mradi wa kuchora ramani za kijiografia
upo chini ya ufadhili wa nci ya Korea kupitia Benki ya Dunia na Umoja wa
Kamisheni ya Afrika.
Na
Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Wizara
ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.
0 comments:
Post a Comment