Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Naibu Waziri Ofisi ya Rasi, Tamisemi Selemani Jafo akitoa maelekezo kwa wataalam wa maji.
Naibu Waziri Ofisi ya Rasi, Tamisemi Selemani Jafo akisikiliza taarifa ya mradi wa maji Mkoyo.
Baadhi ya wajumbe wa kijiji cha Mkoyo pamoja na wataalam wa maji wa manispaa ya Dodoma wakati wa ziara ya kikazi ya Naibu waziri Ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Jafo.
jenerata ya mradi wa maji Mkoyo.
NAIBU
Waziri, Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo amesikitishwa na baadhi
ya wakandarasi washauri wanaosimamia miradi ya maji katika halmashauri
mbalimbali hapa nchini kwa kutofanya kazi yao kwa umakini na hivyo
kuruhusu wakandarasi wa ujenzi wa miradi ya maji kujenga miradi hiyo
chini ya kiwango.
Jafo
alitoa kauli hiyo alipotembelea mradi wa maji katika kijiji cha Mkoyo
ndani ya Manispaa ya Dodoma, ambapo amebaini mkandarasi mshauri wa mradi
huo O&A Co LTD hakuwa makini wakati wa utekelezaji wa mradi huo
kwani imeonekana mradi huo ukiwa na changamoto kadhaa licha fedha
nyingi kutumika zaidi ya milioni 430 kati ya milioni 480 zilizipangwa
kwa mradi huo.
Amesema
wakandarasi hao wamekuwa wakisababisha miradi kujengwa chini ya kiwango
na kusababisha kushindwa kuwapatia maji wananchi kama ilivyotarajiwa. Aidha amebaini kampuni hiyo mshauri huyo ndiye yule yule aliyesimamia mradi kijiji cha Itiso ambao
aliutembelea mradi huo mwezi Agosti mwaka huu na kukumbana na changamoto nyingi.Kufuatia
hali hiyo, Jafo amemuagiza Mkurugenzi Msaidizi wa Ofisi ya Rais
Tamisemi Mhandisi Enock kwa shirikiana na wahandisi wa maji wa
halmashauri za mkoa wa Dodoma kufanya tathmini ya miradi yote ya maji
inayosimamiwa na mshauri huyo ili Ofisi ya Tamisemi ifanye maamuzi
sahihi.
Aidha
amesema serikali haitaweza kuvumilia endapo ikibainika mshauri wa
miradi hiyo ameshindwa kuisaidia serikali katika miradi ya maji
anayoisimamia.
Naibu
waziri Jafo amezitaka kampuni zote za washauri waelekezi kutimiza
wajibu wao katika kusimamia miradi ya maji kwani wananchi wamekuwa
wakitaabika sana kutokana na kero ya maji ilihali wao wamechukua dhamana
ya kusimamia miradi hiyo ya serikali.
0 comments:
Post a Comment