Masoud Masasi,Dodoma yetu BlogMAMLAKA ya Majisafi na Majitaka mjini Dodoma(DUWASA)imemwomba Naibu waWaziri wa Maji kuwasaidia nguvu ili kuweza kulipwa kwa malimbikizo yaAnkara ya maji ya sh 225.6 milioni wanazodai kwa taasisi za kijeshimkoani hapa pamoja na hospitali ya mkoa.Taasisi hizo ambazo zinadaiwa kwa muda mrefu kutokana na kuwa wadaiwasugu ni jeshi la Polisi,Magereza na Jeshi la Kujenga taifa pamoja nahospitali ya Mkoa wa Dodoma.Akizungumza wakati wa ziara ya Naibu waziri kwenye mamlaka hiyoBinilith Mahenge,kaimu mkurugenzi wa Duwasa Sebastian Warioba amesemataasisi hizo zimekuwa wadaiwa sugu kwa kipindi cha miezi sita.Warioba amesema katika malimbikizo hayo jeshi la Polisi mkoani Dodomalinadaiwa sh 95.2 milioni,jeshi la Magereza sh 47.5 huku jeshi laKujenga Taifa(JKT)lenyewe likidaiwa sh 51.3 ambapo amesema hospitaliya mkoa yenyewe ikiwa inadaiwa sh 31.6 milioni madeni hayo yakiishiajuni 2012.Amesema pamoja na kuwapa taarifa kuhusu madeni hayo lakini badohawajalipwa kiasi chochote cha pesa ambapo alimwomba naibu wazirikuwasaidia ili kuweza kupatiwa fedha hizo.Warioba amezitaja baadhi ya taasisi ikiwemo Ikulu,Bunge,Chuo Kikuucha Dodoma (UDOM) kuwa zinaongoza kwa ulipaji mzuri wa Ankara ya majikwa mkoa.Akizungumzia suala hilo naibu waziri Mahenge alisema atalishughulikiasuala hilo kwa kuzungumza na waziri husika ili kuona deni hilolinalipwa ambapo pia aliwataka wasikatie maji taasisi hizo.
Home »
» DUWASA YAOMBA NGUVU NAIBU WAZIRI KUDAI MAMILIONI WANAYOZIDAI TAASISI ZA KIJESHI
0 comments:
Post a Comment