Masoud Masasi- Dodoma yetu BlogBAADHI ya wakulima wa zao la Alizeti wamesema kitendo cha kuongeza kwakodi ya mafuta ya kupikia yanayoingizwa kutoka nje ya nchi kutawafanyazao hilo sasa kuweza kupanuka kibiashara.Walisema serikali imeweza kusikia kilio cha cha siku nyingi kwanimafuta hayo yalikuwa yakiingizwa chini kwa kodi ndogo jambolinalofanya kuuza kwa bei ya chini ikilinganishwa na mafuta yaalizeti.Hayo yalibainishwa jana mjini Dodoma na wakulima wa zao la Alizetiwakati wa warsha ya siku ya mbili ya wakulima ambao ni wadau taasisiya Rural Livelihood Development Company(RLDC)inayojihusisha nashughuli za kilimo na ufugaji.Wakulima hao wamesema moja ya changamoto kubwa waliyokuwa wanakutananayo ni soko la mafuta ya alizeti kuwa dogo kutokana na mafuta mengineyanayoingizwa nchini kuuzwa kwa bei nafuu.Rosemarina Jima mkulima wa zao hilo kutoka mkoani Singida amesema kwasasa wataweza kushindana katika soko la mafuta ya alizeti na mafutamengine kutokana na uongezeko la kodi kwa mafuta hayo yanayotoka njeya nchi.Amesema kwa kawaida mafuta ya alizeti yalikuwa juu sana kwenye sokolake ikilinganishwa na mafuta na hayo ambayo kwenye soko lake yalikuwayakiuzwa kwa bei ya chini hatua iliyofanya mafuta ya alizeti kutouzikakwa kiwango kikubwa.
Home »
» wakulima alizeti wasema kuongezwa kwa kodi kwa mafuta yanayoingizwa kutoka nje itasaidia kuwepo kwa soko la uhakika
0 comments:
Post a Comment