Masoud Masasi, Dodoma Yetu
TAASISI ya Taifa ya utafiti wa taifa ya mifugo(TALIRI) imesema mabadiliko ya tabia ya nchi yameathiri kwa kiasi kikubwa shughuli za utafiti pamoja na uzalishaji katika kituo hicho.
Hayo yalibainishwa juzi mjini Dodoma na mkurugenzi wa taasisi hiyo Dk David Sendalo wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari juu ya changamoto zinazoikumba kituo hicho cha taifa cha utafiti.
Hayo yalibainishwa juzi mjini Dodoma na mkurugenzi wa taasisi hiyo Dk David Sendalo wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari juu ya changamoto zinazoikumba kituo hicho cha taifa cha utafiti.
Sendalo amesema kipindi cha nyuma shughuli za uzalishaji na utafiti zilikuwa kwa ufanisi mkubwa kuliko ilivyo sasa kutokana na mabadiliko ya tabia ya nchi ambayo yameathiri kwa kiasi kikubwa taasisi hiyo.
Mkurugenzi huyo alibainisha kuwa mabadiliko hayo ya hali ya hewa yaliyoathiri shughuli hizo yalitokana na upatikanaji mdogo wa mvua ambao hauzingatii misimu ya mvua jambo ambalo amesema ni kikwazo
kikubwa kwao.
Amesema jambo hilo limefanya mifugo kushambuliwa na magonjwa na kusababisha kufa tofauti na kipindi cha nyuma ambacho kilikuwa na hali nzuri ya hewa na kusababisha uzalishaji kuwa na ubora.
Mkurugenzi huyo aliyataja changamoto nyingine ni magonjwa ambayo yamekuwa tishio kwa mifugo hivi sasa kuwa ni pamoja na ugonjwa wa Lifty valley ambao ulipoteza ngo’mbe wengi sana na ugonjwa wa mapafu ambao umejitokeza hivi sasa kuathiri wanyama wadogo wakiwemo mbuzi.
Dk Sindalo amesema pia elimu inahitajika kwa wafugaji kwa kuwa wamebaini wengi wao hawana mafunzo ya kuweza kufanya shughuli hizo jambo alilosema linasabisha mifugo kutokuwa na afya bora na mingi kufa kutokana na magonjwa.
Blogzamikoa
0 comments:
Post a Comment