Masoud Masasi Dodoma yetu BlogWANANCHI wa kijiji cha Hombolo mkoani Dodoma wameitaka katika katibampya kuwepo kwa kipengele cha sheria ambacho kitamfunga zaidi ya mwakamwanaume au mwanamke atakayeonekana anatembea mitaani amevaa nusuuchi.Wakizungumza katika mdahalo wa kupata maoni ya katiba mpyailiyoendelea katika vijiji vya Manispaa ya Dodoma,wananchi haowamesema sheria hiyo itaweza kukomesha vitendo vya wanaume kutembeawamevaa chini ya makalio nguo zao na wale wanawake wanaovaa nguozinazoonyesha maungo yao ya mwilini.Issa Ali mkazi wa kijiji hicho amesema jamii kwa sasa imekuwa katikahali mbaya haswa kwa vijana kwa kuiga tamaduni za nje na kufanya kuvaanguo ambazo zimekuwa zikiwaacha uchi jamgo alilosema ni hatari kwavizazi vijavyo.Juma Mohamedi amesema ili kuweza kukomesha tabia hiyo kuwepo kwasheria katika katiba mpya ambayo itakuwa ni kosa la jinai kwa mtukuonekana anatembea nusu uchi na kupewa adhabu kali ambayo kifungochake kisipungue mwaka mmoja.Mkazi mwingine Yonadi Mtagwa amesema kama katika katiba mpyakutawekwa kipengele hicho kutaweza kukomesha aibu iliyopo sasa yawanaume na wanawake kutembea nusu uchi kwa kuwa wengi wataogopa mkonowa sheria.Katika mdahalo huo wa kupata maoni ya wananchi juu ya nini kiwepo nakitolewe kwenye katiba mpya zaidi ya wananchi 100 wa kijiji hichowalishiriki katika mdahalo huo ulioandaliwa na mtandao wa asasi zakiraia wa DUNGONET.
Home »
 » WANANCHI WATAKA KWENYE KATIBA MPYA KUWEKWE KWA SHARIA KALI KWA WANAOTEMBEA NUSU UCHI
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment