Home » » Serikali yatakiwa kusaidia wajane, yatima

Serikali yatakiwa kusaidia wajane, yatima


SERIKALI na taasisi zisizo za kiserikali zimetakiwa kulisaidia kundi la wajane na watoto yatima ambalo kwa muda mrefu limekuwa likisahaulika katika jamii.
Wito huo ulitolewa mjini hapa jana na Mchungaji wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT), Dk. William Kopwe alipokuwa akifungua semina ya wajane kitaifa iliyofanyika Chuo Kikuu cha St. John.
Dk. Kopwe alisema wajane na yatima wamesahaulika katika kupatiwa huduma mbalimbali hali inayowafanya kujiona wanyonge na kukata tamaa.
“Kundi hili limesahaulika hata kanisani, wakati hayo ni maagizo ya Mungu kusaidia wajane na yatima…yeye anayeonea wajane na yatima na alaaniwe, haya ni maneno kutoka katika maandiko matakatifu,” alisema.
Alisema umefika wakati kwa Watanzania kumgeukia Mungu na kutimiza maagizo yake kwa kuwasaidia watu hao, ili waweze kushiriki katika fursa mbalimbali.
Mwenyekiti wa huduma inayoshughulika na wajane, yatima na wanafunzi, Witness Msuya, alisema lengo la huduma hiyo ni kuwajenga wanafunzi kiroho, kuwatia moyo na kuwafundisha jinsi ya kutafuta miradi mbalimbali ya ujasiriamali.
Chanzo: Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa