Home » » wananchi wa mpwapwa wailalamikia serikali yao kwa kujengewa makaburi fekiwananchi wa mpwapwa wailalamikia serikali yao kwa kujengewa makaburi feki

wananchi wa mpwapwa wailalamikia serikali yao kwa kujengewa makaburi fekiwananchi wa mpwapwa wailalamikia serikali yao kwa kujengewa makaburi feki

Baadhi ya wananchi wa kijiji cha Chipogolo wilayani Mpwapwa mkoa Dodoma, wameulalamikia uongozi wa serikali yao kujenga makaburi feki pasipo kuwashirikisha wahusika wa makaburi hayo.

Wakizungumza  wananchi hao wamemtupia lawama mtendaji wa kijiji YONA MGANGA, na kusema kuwa serikali imeamua kuhamisha makaburi bila kufuata utaratibu.

Akizungumza EMANUELL MKIGA mmoja wa vijana walio pata tenda ya uhamishaji wa makaburi hayo ameelezea jinsi zoezi hilo la ujenzi wa makaburi feki lilivyofanyika katika kijiji hicho kwa kusema kuwa  walilipwa shilingi elfu tisa kwa ajili ya ujenzi.

ARFEDI NDEGEULAYA Mwenyekiti wa kijiji cha mpwapwa amethibitisha kuwepo kwa tatizo hilo na kusema kuwa yeye anafanya jitihada mbalimbali ili kumaliza tatizo hilo katika kijiji chake.
Chanzo;jiachie blog


0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa