Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Mtandao wa wanawake waharakati wa katiba wamelitaka bunge maalumu la katiba kuongeza usawa wa jinsia kuwa tunu ya taifa.
Msemaji wa mtandao huo, Halima Sharif, alisema kwenye rasimu ya
katiba inayojadiliwa bungeni zimetajwa tunu saba, hivyo wanataka usawa
wa kijinsia uongeze kwenye orodha hiyo.
Tunu hizo ni utu, uzalendo, uadilifu, uwajibikaji, uwazi, umoja, pamoja na Kiswahili.
“Tunalitaka bunge liongeze usawa wa kijinsia ili kuwiana na mkakati
wa ushiriki wa 50 kwa 50 baina ya wanawake na wanaume, unaotajwa
kwenye Protokali ya Maputo inayohimizia ushirikishwaji na fursa sawa kwa
wote”, alisisitiza.
Mwanamtandao mwingine, Asseny Muro, alisema mfumo wa sheria haumpi mwanamke fursa ya kushiriki shughuli za kimaendeleo.
“Mchakato wa katiba uzingatie usawa wa jinsia katika kumilikishwa
rasilimali mbalimbali ikiwamo ardhi kwa sababu imekuwa ni moja ya sababu
ya kumgandamiza mwanamke,”alisema Asseny na kuongeza kuwa, kuendekeza
mila na desturi potofu kuwa ni chanzo kingine cha kumkandamiza mwanamke.
CHANZO:
NIPASHE
0 comments:
Post a Comment