Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Majuma matatu yamepita tangu kuanza kwa Bunge Maalumu la Katiba,
wajumbe wa Bunge hilo la kihistoria wamekuwa wakifanya kazi moja tu,
kutunga kanuni bora za uendeshaji.
Kamati ya Kanuni, ikiongozwa na Profesa Costa
Ricky Mahalu imejitahidi kufanya kazi nzuri, hasa ya kuwarudisha wajumbe
katika Sheria ya Mabadiliko ya Katiba.
Sina tatizo sana na sehemu kubwa ya kanuni hizo,
tatizo langu ni kundi la wajumbe wanawake kudai haki zaidi kwenye kanuni
hizo hata ambazo sasa zinakwenda kinyume na sheria na Katiba ya nchi.
Nilifuatilia kwa karibu sana michango ya baadhi ya
dada zangu na wengine ambao nadiriki kusema wana umri sawa na mama
yangu, lakini haki walizozidai zilivuka mipaka.
Wakati wakichangia Rasimu ya Kanuni, baadhi ya
wajumbe wa jinsi hiyo walikwenda mbali na kutaka Mwenyekiti wa Bunge
akiwa mwanaume, makamu wake awe mwanamke.
Hawakuishia hapo, kwani walitaka hata kama mwenyekiti wa Kamati ya Bunge anakuwa mwanaume, basi makamu wake awe mwanamke.
Hoja kubwa waliyoijenga hapa ni kwamba wanataka
usawa wa jinsia, hata kama kwa kudai haki hiyo inakwenda kinyume na
Sheria ya Mabadiliko ya Katiba au Katiba ya Nchi ya mwaka 1977.
Ni vizuri nikatumia fursa hii kuwarudisha wajumbe
waliokuwa wakipaza sauti, huku wakitoka mapovu wakidai usawa huo, juu
kuwapo kwa kifungu cha 23 (A) cha sheria ya mabadiliko ya katiba sura ya
83.
Sehemu ya pili ya kifungu hicho inasomeka hivi:
‘Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba,
watachaguliwa kutoka miongoni mwa wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba.”
Kifungu hicho hicho kinaeleza zaidi kuwa “endapo
mwenyekiti anatoka upande mmoja wa Jamhuri ya Muungano, basi makamu wake
atakuwa mtu anayetoka upande mwingine wa Jamhuri ya Muungano”.
Sifa ya mtu anayestahili kushika wadhifa huo
imeainishwa katika kifungu kidogo cha tatu cha sheria hiyo kuwa atapaswa
kuwa amehitimu shahada kutoka chuo kikuu kinachotambulika.
Sheria hiyo pia inataka mwenyekiti huyo au makamu
wake, awe amethibitika kuwa na uzoefu na ujuzi wa kuongoza mihadhara au
mabaraza. Hakuna jinsia hapo.
Kwa mtazamo wangu naona haikuwa sahihi kwa wajumbe kutaka viongozi kuchaguliwa kwa jinsia.
Chanzo;Mwananchi
Kwa mtazamo wangu naona haikuwa sahihi kwa wajumbe kutaka viongozi kuchaguliwa kwa jinsia.
Chanzo;Mwananchi
0 comments:
Post a Comment