Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Wajumbe wa Bunge la Katiba, ambao ni Wanachama wa Umoja wa
Katiba ya Wananchi (Ukawa), wanatarajia kufanya uchaguzi wa kudumu
Jumapili hii kupata viongozi wapya.
Katibu wa muda wa Ukawa ambao siku za karibuni,
wamejipatia umaarufu mkubwa katika Vikao vya Bunge la Katiba, Julius
Mtatiro, aliliambia gazeti hili kuwa uchaguzi huo, utafanyika kwa
kujumuisha makundi yote.
Mtatiro alisema hadi sasa Ukawa ina wanachama 286
kutoka vyama vyote vya siasa na katika kundi la wajumbe 201 walioteuliwa
na Rais Jakaya Kikwete.
“Kwa muda mfupi tangu tumeanzisha Uwaka kwa ajili
ya kutetea maoni ya wananchi yaliyopo kwenye Rasimu ya Katiba tumekuwa
na mafanikio makubwa katika kusimamia kanuni za Bunge”alisema Mtatiro.
Alisema moja ya mafanikio ni kuhakikisha
Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Jaji Joseph Warioba,anapata
muda wa kutosha kuwasilisha rasimu tofauti na ilivyokuwa imepangwa.
Alisema katika uchaguzi huo, wanatarajia kupata
viongozi kutoka katika makundi yote ambayo yamewakilishwa katika Bunge
la Katiba.
Viongozi wa muda ambao wataongoza Ukawa ni
Mwenyekiti James Mbatia, Katibu Julius Mtatiro makamu Mwenyekiti ni
profesa Ibrahimu Lipumba na viongozi wengine ni Freeman Mbowe na Tundu
Lissu ambao wamekuwa wakiitisha vikao mara kadhaa bungeni
Chanzo;Mwananchi
Chanzo;Mwananchi
0 comments:
Post a Comment