Home » » Lembeli: Bado naililia Tanganyika

Lembeli: Bado naililia Tanganyika

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Mjumbe wa Bunge Maalumu la Katiba, James Lembeli ameapa hatakuwa tayari kubadili msimamo wake kuhusu Muundo wa Muungano badala yake atasimamia kauli yake kwamba ukamilifu wa Tanzania ni kuwa na Serikali ya Tanganyika.
Lembeli alisema kuwa, kauli aliyoitoa kuhusu kura ya siri itabaki hivyo hadi mwisho wa kuchangia Rasimu ya Katiba kwa kuwa ndicho anachokiamini.
Mwishoni mwa wiki wajumbe walipitisha kanuni ya 37 na 38 ambazo zilileta utata mkubwa ndani ya Bunge la Katiba hadi ikapendekezwa kuwapo kura mbili kwa wakati mmoja.
Hata hivyo, wakati hayo yakitokea, Lembeli hakuwapo ndani ya Bunge hivyo hakuweza kupiga kura kuonyesha msimamo wake.
 “Ni ukweli kwamba siku ya upigaji wa kura sikuwapo, lakini kama ningekuwapo bado ningeendelea kusimamia msimamo wangu huo hadi mwisho kwamba  nataka kura ya siri,” alisema Lembeli.
Alisema suala la kura ya siri ndio msimamo wake ambao amekuwa nao siku zote akiamini kuwa ndio utakaotoa haki kwa wananchi wa Kahama kufikisha mawazo yao.
Kuhusu tetesi kuwa wana CCM wanaopinga uwapo wa kura ya wazi wanaweza kushughulikiwa, mjumbe huyo alisema: “Hakuna wa kumshughulikia mwenzake, isipokuwa ni Mwenyezi Mungu peke yake mwenye uwezo huo.”
Kwa mujibu wa Lembeli, anacholilia katika kura ya siri ni kutaka Tanganyika isimame na kupewa hadhi yake hata kama si kwa masuala yote.
 Chanzo;Mwananchi

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa