Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Ndugu wa kuzaliwa ambao ni wajumbe wa Bunge la Katiba, John na
Isaack Cheyo, juzi waliongozana kutoa tamko linalozungumzia Mkutano wa
Rais Jakaya Kikwete na uongozi wa vyama vya siasa.
John Cheyo ni Mbunge wa Bariadi Mashariki (UDP) na
Isaack ni mdogo wake na mwanachama katika chama hicho ambaye naye
aliteuliwa na Rais kuwa miongoni mwa wajumbe wa Bunge la Katiba.
Juzi, Cheyo mkubwa ambaye ni Mwenyekiti wa Kituo
cha Demokrasia nchini (TCD), alikutana na waandishi wa habari
kuwajulisha kuwa Rais Kikwete amekubali ombi la vyama vya siasa la
kukutana naye ili kujadili kuhusu mchakato wa Katiba.
Cheyo alisindikizwa na mdogo wake pamoja na Fahm Dovutwa wa UPDP, lakini msemaji alikuwa ni Cheyo mkubwa.
Kumekuwapo na malalamiko kutoka kwa baadhi ya watu
ambao huwatuhumu wanasiasa kuwa wanabebana katika kupeana nafasi za
uongozi ndani ya vyama na hata katika nafasi za uwakilishi.
Chanzo;Mwananchi
0 comments:
Post a Comment