Home » » OMBAOMBA: IJUMAA NI SIKU YA MSHAHARA KWETU

OMBAOMBA: IJUMAA NI SIKU YA MSHAHARA KWETU

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

WAKATI Tatizo la Ombamba nchini limekuwa sugu huku jitihada za kulitatua bado hazijafanikiwa, Ombaomba mkoani Dodoma wamekiri kuwa  Ijumaa yoyote kwao wameifanya kuwa siku ya mshahara hivyo watendaji wasiwabughudhi.
Wakizungumza wakiwa kwenye msururu wa kugawiwa ‘Uji na Unga kibaba kimoja mkoani hapa jana, pembeni kidogo mwa Msikiti wa Nunge karibu na Hoteli ya Wimpy, Ombaomba hao walidai, wanataka wasibughudhiwe kwa sababu siku hiyo ni siku ya malipo na mshahara kwao.
Walipoulizwa ni nani anayewalipa mshahara wakati hawafanyi kazi ila kuomba, walijigamba wakisema kama wafanyakazi wengine wanavyolipwa na waajiri wao, nao wana Waajiri wao barabarani ambapo watu wenye mapenzi mema na roho nzuri, huwapatia chochote walichonacho.
“Kama ninyi mnavyodai na kuandamana mnapocheleweshewa mishahara, hata sisi siku ya Ijumaa ambapo Wa-Islamu na watu wenye mapenzi mema, hutupatia zaka zao ikiwa ni pamoja na Chakula, Fedha na Nguo.
Tunashangaa Askari na Wafanyakazi wa Halmashauri ya Mji wa Dodoma wanapotuondoa barabarani wakati tupo kwenye meli moja ya kujitafutia riziki! Tofauti yetu ni kwamba, wao wanaomba kwa kufanya kazi, sisi tunaomba kwa kusaidiwa”.alisema Mama aliyejita Mdala Roda.
Utafiti uliofanywa 2013 na  Shirika linashughulika na masuala ya Familia na Afya (FHI360) chini ya mradi wa Pamoja Tuwalee; Kati ya watoto 332 waliohojiwa, asilimia 35.5 sawa na watoto 118, walibainika wanatoka Dodoma; 
Chanzo:Tanzania Daima 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa