Home » » WAZIRI WA NISHATI NA MADINI AKAGUA MIRADI YA REA MPWAWA.‏

WAZIRI WA NISHATI NA MADINI AKAGUA MIRADI YA REA MPWAWA.‏

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Na Urban Epimark,Dodoma
Wito umetolewa kwa Halmashauri zote nchini kupanga utaratibu wa kumilikisha na kutoa leseni za uchimbaji madini kwenye serikali za vijiji kwenye maeneo yatakayogundulika kuwa na madini ili mapato hayo yaweze kusaidia serikali za vijiji kuendeleza huduma za kijamii.
Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Nishati na Madini Mh George Simbachawekene, ambae pia ni Mbunge wa Kibakwe alipokuwa akitembelea maendelea ya usambazaji umeme vijijini (REA) hivi karibuni katika wilaya ya Mpwawa.
Waziri akiambatana na maofisa ya Wizara ya hiyo upande wa Madini na Nishati, alisema maeneo mengi kwa sasa yamegundulika kuwepo na madini mbalimbali yakiwamo yenye thamani ya juu na ya chini ikiwamo wilaya ya Mpwawa. Amezishauri serikali zote za vijiji nchini kushirikiana na maofisa wa madini walio katika kanda zao ili wawasaidie kuyatambua madini hayo na kuwapatia leseni za kuyachimba kama vijiji na si mtu binafsi.
Nae Kamishna wa Madini Kanda ya Kati, Injiania Sothenes Massola aliwaambia wananchi wa maeneo hayo ya Mpwawa kuwa, wilaya yao imegundulika kuwa na baadhi ya madini mengi yakiwamo shaba, rubi na chokaa pamoja na mawe, mchanga na udongo mzuri kwa ajili ya ujenzi wa barabara na majumba ambazo zote ni madini kulingana na utaratibu. Amesema, Ofisi ya Madini Kanda ya Kati itaanda ziara ya kutembelea wanakijiji wote maeneo hayo hususani yenye madini na kutoa elimu ya jinsi ya kuyatambua madini hayo na taratibu za kupatiwa leseni ili wasidhulumiwe na wajanja wachache.
Wananchi wa wilaya hiyo ya Mpwawa walivutiwa na ziara ya hiyo ya Waziri na kumwomba awasaidie haraka ili vijiji vyao viweze kupatiwa leseni na elimu ya kutambua madini hayo. Walieleza kwamba endapo watapatiwa uelewa wa shughuli za madini, vijana wengi watajihusisha na kazi hiyo na kuondoa tatizo la umaskini unaolikabili taifa.
Waziri pia amelipongeza shirika la umeme nchini, TANESCO kwa kusimamia vizuri kasi ya usambazaji umeme vijijini kwa kushirikiana na wakala wa umeme vijiji yaani REA.
Meneja wa Tanesco Kanda ya Kati Injiani Joeli Kuandika, alimweleza Waziri kwamba, watahakikisha kasi ya usambazaji umeme maeneo yaliyokusudiwa wilaya ya Mpwawa yatawaka umeme kama ilivyopangwa kwa kushirikiana na REA kwani hadi sasa kasi ya usambazaji inaenda vizuri.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa